Tafakari Nasi

Wednesday, 27 February 2013

Upendo wa MUNGU kwa Wanadamu




Isaya 53:3-7 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote. Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake. 



Posted by Robby at 17:41
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Followers

Blog Archive

  • ►  2015 (4)
    • ►  January (4)
  • ►  2014 (20)
    • ►  December (3)
    • ►  July (13)
    • ►  June (4)
  • ▼  2013 (2)
    • ▼  February (2)
      • MUNGU ni Nani?
      • Upendo wa MUNGU kwa Wanadamu
  • ►  2011 (2)
    • ►  September (2)
Watermark theme. Theme images by konradlew. Powered by Blogger.